Sunday, July 8, 2012

Nikki Mbishi amemdiss One The Incredible?



Okay, tunafahamu kuwa Nikki Mbishi na One The Incredible ni watoto waliokuzwa na baba mmoja kimuziki (MLAB Studio) chini ya producer Duke Touchez.

Mara nyingi wamekuwa wakifanya ngoma pamoja. Lakini kitu kimoja tu ambacho Nikki hakifurahii kila asikiapo jina la One! Ni kwamba wasanii wengi sasa hivi wanamuiga sana One katika uandishi na flow.

“EMCEES wengi wanataka kurap kama ONE The Inkredibo,hawajui kuwa Maalim Nash a.ka.Nash Mcee pia ni mcee mwenye mitindo hatari na hawajifunzi kupitia kwake#WAMEENEA KWENYE BOX NDO MAANA HAWAWEZI KUFIKIRI NJE YA BOX#,” ameandika leo jumapili kupitia Facebook.


Maalim Nash (kulia), mshikaji na Nikki Mbishi

Kwanini tunauliza kama Nikki amemdiss One The Incredible? Okay kama ulikuwa hujui ni kuwa kipindi Nikki Mbishi anatoka, alikuja na style yake ya kipekee ya uandishi na mituo kwenye vina vyake. Kwa muda mfupi sana style hiyo ikawaambukiza wasanii wengi wachanga. Kila mmoja akaanza kuandika na kutua kwenye vina kama yeye. 


Nikki, Stereo, One na washkaji

Kipindi hicho One alikuwa hajulikani kabisa. One amekuja kujulikana kwenye ngoma waliyofanya yeye,  Nikki,Godzilla na kumshirikisha Belle 9 kwenye chorus,’Kila Siku’. Hapo ndipo akagundulika msanii mwingine hatari kutoka MLAB!

One alipoachia debut single yake iliyoitwa The Incredible ndipo wakampa salute zaidi na hata kutishia crown ya Nikki Mbishi. Hata hivyo ukweli ni kwamba One aliwahi kukiri kuwa anamuogopa sana Nikki Mbishi kwa uandishi!

Then tunapoona status kama hiyo iliyoandikwa na Nikki hasa kwa kumsifia Nash mc dhidi ya One, it sounds like a potential diss to us! Let’s wait.  

No comments:

Post a Comment