Monday, August 20, 2012

Justin Bieber na Lady Gaga wamuunga mkono Beyonce kwa kampeni ya Humanitarian Day


Justin Bieber, Lady Gaga na Michelle Obama wamempa support Beyonce kwenye kampeni yake ya kimataifa ya World Humanitarian Day ambayo Beyonce aliiadhimisha kwa kuzindua video yake ya wimbo wake I Was Here, iliyochukuliwa wiki iliyopita kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York.

Kampeni hiyo inawataka watu kuwasaidia wengine kama kupika chakula kwa wasiojiweza ama kutoa misaada.

Lengo ni kusambaza jumbe bilioni moja za matumaini.

Wengine wanaoshiriki ni Rihanna, Shakira, Jay-Z, Gwyneth Paltrow na Chris Martin.


No comments:

Post a Comment